Disemba 10, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kiliungana na jamii ya ulimwengu kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Haki za Binadamu. Katika maadhimisho hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali mgeni rasmi alikuwa ni Waziri Mkuu wa zamani, Jaji Mstaafu Joseph Warioba.
Maadhimisho haya yaliambatana na kauli mbiu ya Haki ni ‘Maendeleo, Simamia Haki’ – ikiwa na lengo la kuhimiza umuhimu wa kulinda haki za binadamu katika kuchagiza maendeleo na kuonesha kwamba haki za binadamu na maendeleo haviwezi kutenganishwa.
Hotuba ya Mgeni Rasmi, Jaji Mstaafu Warioba ililenga kuonesha umuhimu wa kulinda amani katika kulinda na kudumisha haki za binadamu, ikitaja kwamba amani ni tunda la haki. Mhe. Warioba kupitia hotuba yake ameonesha kusikitishwa na vitendo vinavyochochea vurugu na uvunjifu wa amani vilivyojitokeza katika uchaguzi mkuu wa Oktoba. Mhe. Warioba amewataka wanasiasa kutimiza wajibu wao wa kisiasa kujenga jamii isiyo na ubaguzi wa kisiasa ambao kwa mujibu wake unaweza kuchochea uvunjifu wa amani ambayo imejengwa kwa muda mrefu na kwa juhudi kubwa.
Soma zaidi hotuba ya Mhe. Warioba hapa
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.
LEAVE A REPLY
Your email address will not be published.