Wadau wa vyombo vya habari na wanaharakati wa haki za binadamu wamekutana Februari 14, 2018 katika ofisi za Makao Makuu ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kujadili namna bora ya kutatua ongezeko la ukandamizwaji wa uhuru wa kujieleza na uhuru wa kukusanyika ili kuongeza ushiriki wa wananchi katika masuala ya haki za kiraia na kisiasa.
Mkutano huo umewakutanisha wawakilishi kutoka asasi mbalimbali ikiwemo Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), TWAWEZA, Mfuko wa Wanawake Tanzania, Policy Forum, WiLDAF, Umoja wa Vyama vya Siasa (TCD), Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Tanzania (CHRAGG), TGNP, pamoja na wadau wa vyombo vya habari kutoka Baraza la Habari Tanzania (MCT) na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF. Washiriki wamekubaliana kudumisha ushirikiano katika kushawishi Serikali kufanya maboresho kisheria na kiutendaji ili kulinda uhuru wa kujieleza na uhuru wa kukusanyika kwa lengo la kudumisha ushiriki wa wananchi katika ujenzi wa taifa.
Kupitia kikao hicho, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kimetambulisha mradi mpya ambao unalenga kuongeza uelewa wa wananchi juu ya sheria zinazosimamia masuala ya habari na mawasiliano sambamba na kuongeza ushiriki wa wananchi katika masuala ya kiraia na kisiasa.
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.
LEAVE A REPLY
Your email address will not be published.